Home NEWS NI FURAHA BAADA YA MTOTO MCHANGA ALIYEIBWA KATIKA KAUNTI YA TAVETA KUPATIKANA 

NI FURAHA BAADA YA MTOTO MCHANGA ALIYEIBWA KATIKA KAUNTI YA TAVETA KUPATIKANA 

0

 

Ni wakati wa kupumua kwa mama mzazi na taasisi ya matibabu baada ya mtoto aliyeripotiwa kupotea kupatikana. Maafisa wa polisi huko Voi wamemkamata Christine Kisochi, ambaye anashukiwa kuiba mtoto wa kiume aliyeripotiwa kupotea kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Moi

 

Kulingana na Daktari Bingwa wa moi rufaral hospital huko voi, Jeremiah Shem, mshukiwa, ambaye alijifanya kuwa mjamzito ana aliyetarajiwa kujifungua, aliingia katika wodi moja ya uzazi ya hospitali hiyo akiwa na uchungu wa uongo.Mshukiwa hiyo alidai mtoto ni wake na alijifungua Jumatatu, tarehe 10, katika Hospitali ya Jordan ya Binafsi, lakini hakuweza kutoa nyaraka, akisema kuwa zilikuwa zimepotea.

 

Ambrose Maundu Gerald ambaye ni baba wa mtoto huyo, alipata afueni baada ya mtoto wake kupatikana, akishukuru hospitali na polisi kwa uchunguzi na msaada wao wa kina huku mshikiwa kiwa huyo akizuiliwa katika kituo cha polisi cha Voi kwa uchunguzi zaidi.

Previous articleDAVID MOYA ANGRILY EVICTED FROM KILIMANI HOUSE BY MUMAMA SPONSOR.
Next articleAUDIO | Rapcha – Shytown | download mp3