Home NEWS MWANAHARAKATI AKOSOA UTENDAKAZI WA JAJI MKUU WA KENYA

MWANAHARAKATI AKOSOA UTENDAKAZI WA JAJI MKUU WA KENYA

0

Mwanaharakati wa haki za binadamu Boniface Mwangi amemkosoa Jaji Mkuu Martha Koome kwa tabia yake.  Mwangi alisema kuwa Jaji Mkuu Martha Koome anastahili kulaumiwa kwa kesi kuchukua muda mrefu mahakamani bila sababu thabiti.

Akizungumza siku ya Ijumaa,wiki iliyopita nje ya Mahakama ya Milimani, yeye kama “mwangalizi wa watu” alisema kuwa Koome hapatikani mara nyingi kutekeleza majukumu yake. Mwangi alisema kuwa tabia hiyo inaathiri maafisa na wafanyakazi wengine wa mahakama chini yake, na kuwaeleza kuwa watu hukaa mahakamani kwa masaa mengi wakisubiri majaji na mahakimu ambao wakati huo hawajulikani waliko.

“Kila mara anapokuwa safarini, anahudhuria semina, yuko kwenye safari, yuko nje ya nchi; hafanyi kazi yoyote. Kwa hiyo kama kiongozi wa Mahakama, watu wanaofanya kazi chini yake wanafuata na kuiga tabia yake Kwa sababu ikiwa unakwenda mahakamani na umekaa kwa saa tano, hakuna mtu kwa sababu majaji wako wanakunywa chai au kutembea ovyo,” alisema mwangi.Mwanaharakati huyo amedai kuwa watu wengi huenda mahakamani kufuta huduma ila hukaa kwa muda mrefu bila kuhudumiwa.

Previous articlePastor Kanyari Says He Paid Betty Bayo’s Full Dowry
Next articleAnyang’ Nyong’o biography, age, education, career, family, children, net worth