Home GENERAL Mauzauza Lyrics – Zuchu Ft Khadija Kopa

Mauzauza Lyrics – Zuchu Ft Khadija Kopa

0
Mauzauza Lyrics

Mauzauza Lyrics by Zuchu and Khadija Kopa – Download Mp3 Audio

Mauzauza Lyrics Verse One

Mocco

Funua usijipe mapana
Eti mwili kujitutumusha
Nitakutawanya
Ka bahari na fimbo ya Musa

Umejigeuza soji
Si wa Corolla wala Vogi
Na hilo wala kufoji
Eti lina kupa kodi

Oooh leo nikome Mwenye kiranga Mwenye Kiranga
Hujalijua vizuri litimbwi ni la vanga Mwenye kiranga
Oooh leo boda umeyabana ka Mwenye kiranga
Mi maskini jeuri sitegemei madanga, Mwenye kiranga

Chorus

Mauzauza we mwana mauzauza
Si wamekushindwa kwenu
Walimwengu tutakufunza

Mauzauza we mwana mauzauza
Si wamekushindwa kwenu
Walimwengu tutakufunza

Verse Two 

Unani ni kichwa cha chikichi
Umevaa kinu unatwangia mchi aah

Mwali kigego mwenye nyota ya mitara
Hivi kungwi wako nani wewe? Atajijua
Uso mitego imedoda biashara
Hueleweki si kunguru si mwewe

Wadala ubaki dala mwenzio mimi kibunja
Haufai kwa kafara si puzi wewe ni punja
Umejivesha ubezezi kwa mapana na marefu
Uso na kazi si wa ndala wala peku

Ooooh ondoa ndo mlezi wa hana
We ebu ndege zoa zoa’
Mwali pengo binti mwanya
Tuchunge kwa kudonyoa

Oooh leo nikome Mwenye kiranga, Mwenye Kiranga
Hujalijua vizuri litimbwi ni la vanga Mwenye kiranga
Oooh leo boda umeyabana ka Mwenye kiranga
Mi maskini jeuri sitegemei madanga, Mwenye kiranga

Chorus

Mauzauza we mwana mauzauza
Si wamekushindwa kwenu
Walimwengu tutakufunza

Mauzauza we mwana mauzauza
Si wamekushindwa kwenu
Walimwengu tutakufunza

Mauzauza Lyrics Verse Three

Hahaa kuvaa dera si kazi,
kazi kulikamatia eeh

Utayaweza yangu, yako yanakushinda
Utayaweza yangu, yako yanakushinda
Ooooh tikisa ndole

Utayaweza yangu, yako yanakushinda
Uso kasi mwana wako
Utayaweza yangu, yako yanakushinda
Oooh…nadilidadi

Utayaweza yangu, yako yanakushinda
Usonoga kwa chumvi wala magadi
Utayaweza yangu, yako yanakushinda

Mauzauza Lyrics by Zuchu and Khadija Kopa

ALSO, SING TO – Ashua Lyrics – Zuchu Ft Mbosso

Previous articleAshua Lyrics – Zuchu Ft Mbosso
Next articleRaha Lyrics – Zuchu