Serikali ya Somalia ilizungumza kwa mara ya kwanza kuhusu taarifa ya rais wa Kenya kuhusiana na mzozo wa baharini ambao Mahakama ya Kimataifa ya Haki ilitoa uamuzi wake.Taarifa ya Rais wa Kenya William Ruto ilisema, ‘’Djibouti inapatanisha majirani marafiki katika mzozo wa baharini.’’ Inafahamika kuna juhudi za kutafuta suluhu kwa suala hilo baada ya Kenya kukataa uamuzi wa mahakama ya kimataifa.Mahakama ya Kimataifa ya Haki ilitoa uamuzi ulioiunga mkono Somalia mnamo Oktoba 2021, baada ya miaka kadhaa ya pande zote mbili kudai – zinamiliki sehemu ya bahari ambayo inasemekana ina mafuta.
Somalia imesema hakuna makubaliano yataafikiwa kuhusu mzozo wa mpaka wa bahari kati yake na Kenya. Waziri wa Nchi anayeshughulikia mambo ya nje wa Somalia, Ali Omar Mohamed (Ali Balcad), alizungumza mbele kamati ya bunge inayohusika na masuala ya kigeni Djibouti haijasema rasmi kuwa inapatanisha kati ya Somalia na Kenya.Mzozo wa mpaka wa baharini kati ya nchi hizo mbili umekuwa ukiendelea kwa muda na kusababisha mzozo wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili. Ni ardhi ya pembetatu katika Bahari ya Hindi yenye ukubwa wa maili 100,000.Waziri wa Habari wa Somalia wakati huo, Osman Abokor Dube, ambaye sasa ni seneta katika baraza la juu, alisema kwenye akaunti yake ya Twitter, amefurahishwa na uamuzi huo na anawapongeza Wasomali wote kwa kurejeshewa ardhi yao.
Kwa muda wa miaka 10 iliyopita, Kenya imekuwa ikidai kuwa mstari wa mpaka unahamia mashariki, na inazingatia mpaka kati ya nchi hizo mbili kuwa baharini.Lakini Somalia ilisema katika mahakama kwamba mstari wa mpaka wa bahari sio lazima kufuata moja kwa moja mpaka wa nchi kavu wa nchi hizo mbili.Majaji 14, walioketi kuamua mzozo huo walikuja na mpaka mpya unaogawanya bahari inayozozaniwa, ingawa sehemu kubwa ilienda Somalia.Rais wa zamani wa Somalia, Mohamed Abdullahi Mohamed.