Home NEWS Acha Iwe Lyrics – NEDY MUSIC

Acha Iwe Lyrics – NEDY MUSIC

0
Acha Iwe Lyrics

Acha Iwe Lyrics by NEDY MUSIC

Verse One

Umenifuta alama ya upendo
Kwenye penzi langu
Tena ukashindwa kuficha matendo
Kwenye mboni zangu

Najihisi moyo una ganzi
Ngumu kufika safari yangu
Kinywa kibogoyo silambi
Wala kutafuna

Aliniteka akili yangu
Nikazama mazima mazima
Mwisho wa siku ikala kwangu
Kichwa ikabaki na jina

Oooh yanauma
Ndio maana

Kila siku shida shida
Tajiri wa huzuni
Ndonda limekosa tiba
Nitapona lini?

Mie eh

Chorus

Acha iwe, we acha iwe, Acha iwe,
Bora nibaki mwenyewe
Acha iwe, we acha iwe, Acha iwe,
Bora nibaki mwenyewe

Verse Two

Nilishapona kidonda
Ona kaja kukitonesha
Kinywa nong’ona kupenda
Nakosa jibu kuwtwa nakesha

Naumwa kuwaza eh
Huenda pengine moyo hujaridhia
Nyota angaza eh
Mizani nipime wapi nafsi itatulia

Ama ni nuksi mikosi
Nyota ya punda yangu kubeba mizigo
Nakazana kufosi
Cha jana kuvunda kwangu mi nishazoe

Kila siku shida shida
Tajiri wa huzuni
Donda limekosa tiba
Nitapona lini?

Mie eh

Chorus

Acha iwe, we acha iwe, Acha iwe,
Bora nibaki mwenyewe
Acha iwe, we acha iwe, Acha iwe,
Bora nibaki mwenyewe

Last 

Kila siku shida shida
Tajiri wa huzuni
Donda limekosa tiba
Nitapona lini mie

Acha Iwe Lyrics by NEDY MUSIC

ALSO, SING TO – Dakika Lyrics – KUSAH

Previous articleDakika Lyrics – KUSAH
Next articleNHIF Linda Mama Registration and Benefits